Makumi ya mashabiki wa kilabu ya Arsenal katika kaunti ya Garissa walijitokeza kwa wingi ili
kusherehekea ushindi wa kilabu ya kuitwa kombe la Epl msimu huu.
Wakizungumza mjini Garissa mshabiki hao wakiongozwa na Dickson Odhiambo waliisifia
kilabu hiyo kwa kutwaa ubingwa huo, huku wengi wao wakisema kuwa kwa kipindi cha
miaka 22 wamekuwa wakiisubiria ushindi huo na sasa maombi yao yamejibiwa na mungu.
Klabu hiyo ya Arsenal kwa sasa wameshinda taji hilo mara nne huku wakitwaa kombe hilo la
Epl mwaka wa 1997 kwa mara ya kwanza,kisha wakafanikiwa vilevile kulishinda taji hilo
mwaka wa 2001,2004 na mwishowe kuitwa tena mwaka huu wa 2025/2026.
