Ahmed Khalif Kuenziwa Kupitia Uwanja wa Wajir
Uwanja mpya wa Wajir sasa utajulikana kama Ahmed Khalif Wajir Stadium baada ya Rais William…
Kiongozi wa taifa ametetea mpango wa serikali wa kujenga kituo cha kuwatenga watu walioathiriwa na virusi vya Ebola katika Kaunti ya Laikipia, akisema hatua hiyo inalenga kuimarisha afya ya umma na uwezo wa Kenya kukabiliana na magonjwa ya mlipuko. Akizungumza na wanahabari katika Ikulu Ndogo ya Wajir, Rais Ruto alisema ujenzi wa kituo hicho ni…
Wanafunzi tisa wa Utumishi Girls Academy wanaodaiwa kuhusika katika tukio la moto ulioteketeza bweni la shule hiyo wamefikishwa katika Mahakama ya Naivasha, wakikabiliwa na tuhuma za mauaji kufuatia vifo vya wanafunzi 16 vilivyotokana na mkasa huo. Katika shauri hilo, upande wa mashtaka umeiomba mahakama kuwaruhusu maafisa wa upelelezi kuwaweka mahabusu washukiwa hao kwa muda wa…
Naibu Gavana wa kaunti ya Taita Taveta Christine Kilalo ametoa wito wa kuimarishwa zaidi kwa ushirikiano wa serikali ya kaunti hiyo na serikali ya kitaifa ili kuweza kupambana na changamoto zinazokumba wakaazi pamoja kufanikisha maendeleo. Kilalo alisema kuwa migogoro ya mashamba, kuimarishwa kwa huduma na kuwaweza wakaazi kimaendeleleo ni baadhi ya maswala ambayo yanastahili kushughulikiwa…
Mawaziri wapya walioteuliwa na Rais Yoweri Museveni wanatarajiwa kupitia mchakato wa uhakiki wa bunge kabla ya kuapishwa na kuanza rasmi kutekeleza majukumu yao serikalini. Mchakato huo utaanza Juni Mosi ambapo kamati za bunge zitawahoji na kutathmini mawaziri hao kwa muda wa siku mbili ili kubaini uwezo wao wa kuongoza wizara walizopangiwa. Baada ya zoezi hilo,…
Mjadala kuhusu mustakabali wa uongozi wa kisiasa katika eneo la Mulembe umechukua mkondo mpya baada ya viongozi kadhaa kuanza kumtaja Katibu Mkuu wa ODM Edwin Sifuna kama mmoja wa viongozi wanaoweza kuiongoza jamii hiyo kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2027. Akizungumza katika Kaunti ya Bungoma, Seneta wa Kakamega Boni Khalwale alisema jamii ya Mulembe inahitaji…
Zaidi ya Wakenya milioni 31.5 wamejisajili chini ya Mamlaka ya Afya ya Jamii (SHA), huku serikali ikisisitiza kuwa mpango huo unaendelea kupanua upatikanaji wa huduma za afya nchini. Akizungumza wakati wa maadhimisho ya Sikukuu ya Madaraka katika Kaunti ya Wajir, Rais William Ruto alisema kati ya waliojisajili, zaidi ya watu 800,000 wanatoka katika kaunti za…
Uwanja mpya wa Wajir sasa utajulikana kama Ahmed Khalif Wajir Stadium baada ya Rais William Ruto kukubali ombi la viongozi wa eneo hilo la kumuenzi mwanasiasa mashuhuri marehemu Ahmed Mohamed Khalif. Hatua hiyo ilitangazwa wakati wa sherehe za Madaraka Day katika Kaunti ya Wajir, ambapo viongozi walieleza kuwa marehemu Khalif aliweka historia kwa kuwa mmoja…
Mahakama Kuu imeizuia kwa muda serikali kuanzisha au kuendesha vituo vya karantini, kutenga au kutibu wagonjwa wa Ebola nchini chini ya makubaliano yoyote na Marekani au taifa lingine la kigeni. Mahakama pia imepiga marufuku kuingizwa nchini, kuhamishwa au kupokelewa kwa watu walioathiriwa au kuambukizwa Ebola hadi kesi hiyo itakaposikilizwa na kuamuliwa. Hatua hiyo ilichukuliwa baada…
Wakulima wa majani chai kutoka maeneo mbalimbali nchini wameibua wasiwasi mkubwa kuhusu ushuru wa asilimia 0.8 uliopendekezwa katika Mswada wa Majani Chai, wakisema hatua hiyo itaongeza mzigo kwa wakulima na kudhoofisha sekta hiyo muhimu ya uchumi. Akizungumza katika kaunti ya Kiambu, mwenyekiti wa kiwanda cha majani chai cha Kagwe, William Muroki Githumbi, alisema wakulima hawakuhusishwa…
Wakazi wa kijiji cha Hidabo kisiwani Lamu wameeleza hofu yao kuhusu athari za kiafya zinazodaiwa kusababishwa na moshi na harufu kali kutoka kwa tanuri ya kuchomea taka za hospitali kuu ya rufaa ya King Fahd. Kijiji hicho chenye zaidi ya wakazi 500 kinapakana na hospitali hiyo, huku wakazi wakisema moshi unaotoka kwenye mtambo huo umeanza…