Rais Ruto yuko Mombasa kupeana hati miliki za ardhi
Rais William Ruto yuko mjini Mombasa kupeana hati miliki za ardhi kwa wamiliki kutoka kaunti za Mombasa, Kwale, Kifili na Taita Taveta.
Rais William Ruto yuko mjini Mombasa kupeana hati miliki za ardhi kwa wamiliki kutoka kaunti za Mombasa, Kwale, Kifili na Taita Taveta.
Mgomo wa magari ya uchukuzi wa umma kupinga bei za mafuta nchini umesitishwa muda wa wiki moja ili kuruhusu mazungumzo zaidi kati ya wamiliki wa magari ya uchukuzi na wizara ya kawi pamoja na washikadau wengine.
Vijana na wahudumu wa bodaboda mjini Marsabit mapema Jumatatu waliungana na wakenya wengine kushiriki maandamano ya kulalamikia ongezeko la bei ya mafuta. Mandamano hayo yalikatiza shughuli za biashara, huku baadhi ya maduka yakisalia kufungwa mapema Jumatatu Maafisa wa polisi walilazimika kutumia vitoa machozi kuwatawanya wandamanaji waliokuwa wakiteketeza magurudumu ya magari na kuziba barabara kuu ya…
Maelfu ya wakenya mapema Jumatatu walilazimika kutembea kuelekea kazini, huku wengine wakisalia nyumbani kwa kukosa usafiri, baada ya kuanza rasmi kwa mgomo unaopinga ongezeko kubwa la bei ya mafuta, huku ikikadiriwa kuwa gharama ya maisha pia huenda ikaongezeka. Naye waziri wa hazina ya kiaifa John Mbadi mapema Jumatatu alisema mgomo huo haukustahili akisema serikali tayari…
Baadhi ya wafanyakazi katika ofisi ya naibu wa rais nchini watarajiwa kujiuzulu huku maafisa wakuu katika ofisi za umma wakionya kuwa wengi wa wafanyakazi huenda wakajiuzulu kabla ya uchaguzi mkuu mwaka 2027, hali iliyosababisha kuongeza kwa mgao wa shilingi milioni 95.4 kwa ajili ya malipo ya watumishi hao wakati watakapoondoka kazini. Suala hilo lilijiri wakati…
Mzozo wa umiliki wa ardhi kwenye mpaka wa kaunti ya Marsabit na Wajir unaendelea kuibua hisia tofauti huku viongozi na wazee wa jamii ya kaunti ya Marsabit wakikashfu ujenzi wa kambi ya usalama katika eneo la Tiitu kwenye mpaka wa kaunit hizo mbili. Mwakilishi wa kike kaunti ya Marsabit, Naomi Jillo Waqo ambaye alizuru eneo…
Mwenyekiti wa bodi ya shirika la kupeana mikopo kwa wakulima (AFC) John Mruttu amewataka wanafunzi kukoma tabia ya uchomaji wa shule katika kaunti ya Taita Taveta kufuatia visa kadhaa kushuhudiwa siku za hivi karibuni. Mruttu pia amewataka washika dau mbali mbali ikiwemo wazazi,walimu sawa na viongozi wa dini kuja pamoja na kuangazia suluhu juu ya…
Kamati ya Seneti kuhusu fedha na bajeti imewasilisha mapendekezo ya marekebisho ya muswada wa ugavi wa mapato wa mwaka 2026 ambayo yanaitaka serikali ya kitaifa kugharamia peke yake upungufu wowote wa mapato utakaojitokeza katika mwaka wa kifedha wa 2026/2027. Marekebisho hayo, yaliyoorodheshwa katika ajenda ya Seneti kabla ya kikao cha Jumanne, yanapendekeza kifungu kipya kinachoeleza…
Mvutano umeibuka kuhusu mpango wa upanuzi wa uwanja wa ndege kaunti ya Wajir huku waamiliki wa ardhi walioathirika wakitishia kuchukua hatua za kisheria dhidi ya mamlaka ya viwanja vya ndege pamoja na serikali ya kaunti hiyo. Wakazi hao wanadai kuna unyakuzi wa ardhi kinyuma cha sheria na kuwa wametengwa katika vikao muhimu vya mashauriano. Zaidi…