Maraga ahimiza Bunge kutekeleza vikao mara moja, akipendekeza mpango wa hatua tatu kupunguza bei ya mafuta
Jaji wa Mahakama Kuu wa zamani David Maraga ameonyesha mshikamano na Wakenya waliokumbwa na kufungwa kwa usafirishaji nchini kote na kuwaomba Bunge kukutana mara moja ili kuidhinisha kifurushi cha hatua ambazo anasema zingelinda umma kutokana na bei za juu za mafuta. Alipendekeza hatua tatu za haraka: kuachilia bidhaa zote za mafuta kwenye VAT, kuondoa kwa…
Usafiri wa umma walemazwa katika miji mikuu na sehemu tofauti nchini, kufuatia mgomo wa magari ya uchukuzi kulalamikia ongezeko kubwa la bei za mafuta ya Dizeli na Petroli
Maelfu ya wakenya mapema Jumatatu walilazimika kutembea kuelekea kazini, huku wengine wakisalia nyumbani kwa kukosa usafiri, baada ya kuanza rasmi kwa mgomo unaopinga ongezeko kubwa la bei ya mafuta, huku ikikadiriwa kuwa gharama ya maisha pia huenda ikaongezeka. Naye waziri wa hazina ya kiaifa John Mbadi mapema Jumatatu alisema mgomo huo haukustahili akisema serikali tayari…
Mlipuko wa Ebola Waongezeka Mashariki mwa DRC
Kulingana na taarifa za hivi karibuni kutoka Africa Centres for Disease Control and Prevention, idadi ya watu waliofariki kutokana na mlipuko mpya wa ugonjwa wa Ebola katika taifa la Democratic Republic of the Congo imeongezeka hadi watu 80, huku takribani visa 246 vikishukiwa kuripotiwa katika jimbo la Ituri mashariki mwa nchi hiyo. Maeneo yaliyoathirika zaidi…
Martha Karua afananisha hali ya sasa ya uchumi na enzi za Moi
Kiongozi wa People’s Liberation Party, Martha Karua, ameilinganisha hali ya sasa ya uchumi nchini Kenya na changamoto zilizoshuhudiwa wakati wa utawala wa hayati Daniel arap Moi, akisema taifa bado limekwama katika mzunguko wa gharama kubwa ya maisha, utawala mbovu na matarajio yasiyotimizwa. Kupitia ujumbe wake kwenye mitandao ya kijamii, Karua alikumbuka hali ya mwezi Juni…
Gachagua ataja mpango wa uagizaji mafuta kuwa “ulaghai”
Kiongozi wa chama cha Democracy for the Citizens Party (DCP), Rigathi Gachagua, ameutaja mpango wa serikali kwa serikali (G-to-G) wa uagizaji mafuta kuwa “ulaghai”, akiishutumu serikali ya Rais William Ruto, pamoja na baadhi ya wafanyabiashara kwa kuwaumiza Wakenya kupitia ongezeko la bei ya mafuta. Akizungumza kabla ya kuondoka kuelekea United Kingdom, Gachagua alisema mzozo wa…
Oburu aitetea ODM kushirikiana na serikali ya Kenya kwanza
Kiongozi wa Orange Democratic Movement (ODM), Oburu Oginga, ametetea ushirikiano wa chama hicho na serikali ya Kenya Kwanza akisema umeleta manufaa ya kisiasa na kiuchumi kwa wafuasi wa chama hicho pamoja na taifa kwa ujumla. Akizungumza wakati wa mkutano wa wadau uliofanyika Nyakach siku ya Ijumaa, mwanasiasa huyo mkongwe alisema uamuzi wa ODM kufanya kazi…
Kuccps yafungua upya awamu ya pili ya maombi ya vyuo vikuu
Shirika la KUCCPS limefungua tena awamu ya pili ya maombi ya kujiunga na vyuo vikuu kwa watahiniwa wa KCSE 2025. Wanafunzi sasa wana nafasi nyingine ya kubadilisha kozi walizochagua au kutuma maombi mapya. Kupitia taarifa iliyotolewa Mei 16, 2026, KUCCPS ilisema mfumo wa maombi utafunguliwa hadi Mei 22, 2026. Awamu ya kwanza ya maombi ilifungwa…
Baadhi ya wafanyakazi katika ofisi ya naibu wa rais nchini huenda wakajiuzulu kujiunga na siasa kabla ya uchaguzi mkuu 2027
Baadhi ya wafanyakazi katika ofisi ya naibu wa rais nchini watarajiwa kujiuzulu huku maafisa wakuu katika ofisi za umma wakionya kuwa wengi wa wafanyakazi huenda wakajiuzulu kabla ya uchaguzi mkuu mwaka 2027, hali iliyosababisha kuongeza kwa mgao wa shilingi milioni 95.4 kwa ajili ya malipo ya watumishi hao wakati watakapoondoka kazini. Suala hilo lilijiri wakati…
Ruto ahakikisha Kenya inaendelea kuongoza katika utafiti wa chanjo
Rais William Ruto alifanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kimataifa ya Chanjo (IVI), Jerome Kim, katika Ikulu ya Nairobi. Rais Ruto alithibitisha tena dhamira ya Kenya kuendelea kushirikiana katika utafiti na maendeleo ya chanjo, majaribio ya kitabibu, ushirikiano wa utengenezaji wa chanjo, kuimarisha mifumo ya udhibiti pamoja na maendeleo ya wafanyakazi. Taasisi hiyo…
